Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed
Gharib Bilal, akipata maelezo ya mradi huo kutoka kwa Mkurugenzi wa
Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Musoma, Gantala Said, wakati wa sherehe za
Kilele cha maadhimisho ya 27 ya Wiki ya Maji zilizofanyika Kitaifa
Mkoani Mara jana Machi 22, 2015.
Imeandikwa na Bigambo Jeje.
Imechapishwa: 20 Januari 2016
MAMLAKA
ya Maji Safi na Taka ya Musoma Mjini (MUWASA) ni moja ya taasisi za umma ambazo
kama zitalipwa ipasavyo na wadeni wake, zinaweza kuboresha utendaji kazi wake
kuliko ilivyo sasa.
Wananchi
wengi wa mji wa Musoma ambao wamekuwa wakilalamikia huduma ya maji, wamekuwa
wakikutana na kauli ya ukata inayoisumbua mamlaka hiyo kutokana na kudai Sh
milioni 560 ambazo hazijalipwa na baadhi ya Taasisi za Serikali mkoani Mara
kutokana na taasisi hizo kulimbikiza ankra za huduma ya maji kwa muda mrefu.



