Jumatano, 26 Novemba 2014

KAMBI YA UPINZANI YAMTAKA KIKWETE AMTIMUE NYARANDU












Pichani kulia ni Mwenyekiti wa halmshauri ya wilaya ya Serengeti Bw. John Ng'oina akiendesha kikao cha baraza hapo jana na kushoto ni Mkurugenzi wa halmshauri hiyo Bi Good Pamba (Picha Na Bigambo Jeje) 






 Picha ya Maktaba ya Waziri Nyalandu.



\


 Rais Jakaya Kikwete anayeombwa amtimue Nyarandu


Na Bigambo Jeje,Serengeti.
 

Kambi ya upinzani  ya baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imemtaka Rais Jakaya Kikwete kumfukuza kazi Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe: Lazaro Nyarandu baada ya Waziri huyo kupingana na ahadi ya Rais ya kujengwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa  Mugumu.

Jumapili, 23 Novemba 2014

KANISA LA WASABATO KAMUNYONGE MUSOMA LAKUNWA NA WARAKA


Pichani ni Mchungaji wa Kanisa la Wasabato Mtaa wa Kamunyonge Muso Stehen Muso akiwa katika moja ya mahubiri yake katika kanisa hilo (Picha na Bigambo Jeje)


Na Bigambo Jeje,Musoma


Kanisa la Waadventista la Wasabato (SDA) la Kamunyonge la Mjini Musoma ambalo ni kanisa Kuu katika jimbo la Mara, limeunga mkono hatua ya serikali ya kufuta utaratibu wa vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini kuwalazimisha wanafunzi kufanya mitihani katika siku zao za ibada hususani siku ya jumamosi.

Jumapili, 9 Novemba 2014

RAIS KIKWETE AFANYIWA UPASUAJI WA TEZI MAREKANI

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania akibadilishana mawazo na mmoja wa madaktari bingwa wa hospitali ya Johns Hopkins muda mfupi kabla ya kufanyiwa oparesheni yake (Picha na IPP Media).



Rais Jakaya Kikwete, amefanyiwa upasuaji wa tezi dume (prostrate) katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Baltimore, Jimbo la Maryland, Marekani.

Jumatatu, 3 Novemba 2014

MFUKO WA BIMA YA AFYA WALETA MADAKTARI BINGWA MARA







Pichani: Meneja huduma za Afya wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Dr Michael Kishiwa akitoa maelezo mafupi wakati wa uzinduzi wa huduma za madaktari bingwa mkoani Mara inazofanyika kwa siku sita mfululizo kwenye hospitali ya serikali ya mkoa ( Picha Na Bigambo Jeje).




Na Bigambo Jeje,Musoma


Serikali mkoani Mara imesema kuwa ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Mwalimu Nyerere unaoendelea kwa fedha za serikali ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete utapunguza kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa huduma za afya toka kwa madaktari bingwa kwa wananchi wa Mara na mikoa ya jirani.

Ijumaa, 26 Septemba 2014

Wagonjwa Mara,Kagera na Manyara wachanga milioni 272

Pichani baadhi ya washiriki ya siku mbili ya kufungwa kwa mradi wa Kaya CCI Mkoani Mara iliyofanyika mjini Musoma jana na leo( Na Bigambo Jeje)


Na Bigambo Jeje Musoma



Wagonjwa wanaoishi na virusi vya Ukimwi toka mikoa mitatu ya Manyara,Mara na Kagera wapatao 23,000 wamekusanya zaidi  ya sh milioni 272 kutokana na michango yao mbalimbali iliyowasaidia kujikimu kiuchumi sanjari na kupata huduma za tiba na kinga kutokana na magonjwa nyemeleziyanayowakabili.

Jumanne, 23 Septemba 2014

MHAGAMA AWATAKA WATANZANIA KUTOWACHAGUA WAPINZANI WA NYERERE

Pichani:Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi bibi Jenisita Mhagama akiwasha mshumaa kwenye kaburi la Baba wa Taifa Mwitongo Butiama. (Na Bigambo Jeje)




Na Bigambo Jeje,Butiama

Naibu wa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bibi Jenister Mhagama amewataka Watanzania kutowachagua viongozi wanaochochea vurugu na fujo kwa wananchi, zenye nia ya kutowesha amani ya nchi iliyoasisiwa na Baba wa Taifa marehemu Mwalimu Julius Nyerere wakati tunapoelekea katika uchaguzi wa mkuu hapo mwakani.

Naibu Waziri Mhagama ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya kuzulu kaburi la Marehemu Mwalimu Nyerere kijijini kwake Mwitongo Butiama wilayani Butiama mkoani Mara ambapo alifuatana na viongozi wa juu wa Chuo Kikuu Huria(OUT) wakiongozwa na Makamu Mkuu wa chuo hicho Profesa Tolly Mbwete.

Jumatatu, 8 Septemba 2014

MIILI YA MAREHEMU WA AJALI MUSOMA YATAMBULIWA

Pichani baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Musoma wakiangalia baadhi ya miili ya marehemu waliokufa katika ajali (Picha Na Bigambo Jeje)