Jumatatu, 27 Julai 2015

MWANASIASA MJINJA AMPISHA MUHONGO UBUNGE MUSOMA VIJIJINI


Na Bigambo Jeje
 
Mwanasiasa mashuhuri toka Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Michael Mujinja amejitoa katika kinyang’anyiro cha ubunge kupitia chama hicho katika jimbo la Musoma Vijijini  huku akisema amejiondoa baada ya kujipima na kuona hana rekodi za uchapazi na utendaji kama alionao Waziri wa zamani wa Nishati na Madini Profesa Sospiter Muhongo anayewania ubunge wa jimbo hilo.

Jumatatu, 26 Januari 2015

KABAKA ALIA NA VIONGOZI WA DINI KUHUSU AJIRA

                                                        Mhe: Joshua Mirumbe - Mkuu wa wilaya ya Bunda




Na Bigambo Jeje,Musoma.


Waziri wa Kazi na Ajira Mhe:Gaudensia Kabaka amewataka viongozi wa madhehebu ya dini kubuni miradi ya maendeleo katika taasisi za kidini wanazoziongoza ili kusaidia kupatikana kwa ajira katika sekta binafsi sanjari na kupunguza umasikini uliokithiri katika jamii hivyo kuisaidia serikali kutekeleza kwa vitendo dira ya taifa ya maendeleo.

Ijumaa, 23 Januari 2015

WAZIRI KABAKA KUONGOZA MAELFU YA WASABATO KAMUNYONGE






                                                   Pichani: Mhe Gaudensia Kabaka.




Waziri wa Kazi na Ajira Mhe:Gaudensia Kabaka January 25 mwaka huu anatarajia kuongoza maelfu ya waumini wa  kanisa la Waadventista la Wasabato la Kamunyonge la Musoma Mjini  ambalo ni kanisa Kuu la Wasabato jimbo la Mara, katika sherehe maalum ya kwaya ya kanisa hilo (Choir day) itakayofanyika katika viwanja vya kanisa hilo.

Jumanne, 6 Januari 2015

ZAHANATI YA MWIRINGO KUWANUFAISHA WATU 4000 KIAFYA



Bigambo Jeje,Musoma

Wananchi zaidi ya 4000 wa vijiji vitatu vya kata ya Busambara katika halmshauri ya wilaya ya Musoma Vijijini mkoani Mara watanufaika na huduma za afya baada ya zahanati inayojengwa katika kijiji cha Mwiringo kwa gharama y ash. milioni 150 kukamilika siku chache zijazo.

Alhamisi, 4 Desemba 2014

VIONGOZI WAPYA WA 2015 KANISA KAMUNYONGE WATAJWA










Kanisa Kuu la Waadventista la Wasabato la Kamunyonge katika Jimbo la Mara limewapata viongozi wake wapya watakaoliongoza kanisa kwa mwaka 2015 huku majina kadhaa yakipanda kwenye nyadhifa za juu na mengine kuhama nafasi moja kwenda nyingine.

Kwa mujibu wa taarifa ya baraza la uchaguzi, aliyekuwa Katibu wa Kanisa kwa miaka mitatu mfululizo Davis Mafuru amepanda na kuwa miongoni mwa Wazee watano watakaoshika hatamu hapo mwakani wakati Mkuu wa Majengo wa 2014 Josiah Magomere akirejea tena kuwa Mzee wa kanisa baada ya kushika wadhifa huo kwa vipindi tofauti tofauti hadi 2013.

Jumatano, 26 Novemba 2014

KAMBI YA UPINZANI YAMTAKA KIKWETE AMTIMUE NYARANDU












Pichani kulia ni Mwenyekiti wa halmshauri ya wilaya ya Serengeti Bw. John Ng'oina akiendesha kikao cha baraza hapo jana na kushoto ni Mkurugenzi wa halmshauri hiyo Bi Good Pamba (Picha Na Bigambo Jeje) 






 Picha ya Maktaba ya Waziri Nyalandu.



\


 Rais Jakaya Kikwete anayeombwa amtimue Nyarandu


Na Bigambo Jeje,Serengeti.
 

Kambi ya upinzani  ya baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara imemtaka Rais Jakaya Kikwete kumfukuza kazi Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe: Lazaro Nyarandu baada ya Waziri huyo kupingana na ahadi ya Rais ya kujengwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa  Mugumu.

Jumapili, 23 Novemba 2014

KANISA LA WASABATO KAMUNYONGE MUSOMA LAKUNWA NA WARAKA


Pichani ni Mchungaji wa Kanisa la Wasabato Mtaa wa Kamunyonge Muso Stehen Muso akiwa katika moja ya mahubiri yake katika kanisa hilo (Picha na Bigambo Jeje)


Na Bigambo Jeje,Musoma


Kanisa la Waadventista la Wasabato (SDA) la Kamunyonge la Mjini Musoma ambalo ni kanisa Kuu katika jimbo la Mara, limeunga mkono hatua ya serikali ya kufuta utaratibu wa vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini kuwalazimisha wanafunzi kufanya mitihani katika siku zao za ibada hususani siku ya jumamosi.